Chama cha Mpira wa miguu nchini (TFF) kimetaja majina ya kikosi cha 
wachezaji 16 kwa ajili ya  maboresho ya timu ya Taifa Stars kati ya 
wachezaji 34 waliokuwa katika kambi ya wiki tatu mjini Tukuyu wilayani 
Rungwe mkoani Mbeya.
Kikosi hicho ambacho kimeelezwa kuwa ni cha maboresho kinatarajia kucheza mechi mbalimbali za kirafiki ya ndani na nje ya nchi.
Akizungumza
 na waandishi wa habari katika Hotel ya Hill View Jijini Mbeya kocha 
msaidizi wa kikosi hicho Salum Mayanga alisema kuwa wachezaji 
walioteuliwa ni pamoja na Mlinda mlango Benedict Tinoko(Mara),Walinzi wa
 kati Emma Namwondo Simwanda(Temeke)Joram Nason Mgeveje(Iringa).
Aliwataja
 walinzi wa pembeni  kuwa ni Omar Ally Kindamba(Temeke)Edward Peter 
Mayunga(Kaskazini Pemba),Shirazi Abdallah Sozigwa(Ilala) na viungo wa 
ulinzi ni Yusuf Suleiman Mlipili(Temeke) na Said Juma Ally(Mjini 
Magharibi).
Wengine
 ni viungo wa ushambuliaji Abubakar Ally
 Mohamed(Kusini Unguja)Hashimu Ramadhan Magona(Shinyanga) ambapo viungo 
wa pembeni ni Omar Athuman Nyenje(Mtwara), Chunga Said Zito(Manyara) na 
washambuliaji wanne ambao ni Mohamed Seif Said(Kusini Pemba)Ayubu Kassim
 Lipati(Ilala) Abdulrahman Othman Ally(Mjini Unguja) na Paul Michael 
Bundala(Ilala).
Pia
 Kocha Mayanga aliwataja wachezaji wawili wa U-20 watakaojiunga na timu 
Serengeti Boys kuwa ni Mbwana Mshindo Mussa kutoka mjini Tanga na Bayaga
 Athanas Fabian kutoka mkoani Mbeya.
Hata
 hivyo alisema kuwa wachezaji 16 waliobaki wataendelea kuwa chini ya 
uangalizi kwa ajili ya kuziba mapengo kwa timu ya Taifa na kwamba 
mchakato wa uteuzi wa wachezaji hao ambao ni mpango mpya wa chama cha 
Mpira wa miguu nchini TFF kuimarisha kikosi cha timu ya Taifa umefanyika
 mara nne ambapo awali jumla ya wachezaji 143 walijitokeza na kuchujwa 
hadi kufikia idadi ya wachezaji 16.
Post a Comment