Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya 
Songea,Prison na Mbeya City za Jijini Mbeya na hatimaye timu ya Kagera 
Sugar DAVID ABDALLAH BURHAN amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali
 ya Bugando jijini Mwanza.
 Kwa mujibu wa kocha wa timu ya Kagera 
Sugar Meck Mexime, Burhani ameugua tumbo siku tatu zilizopita walipofika
 Kagera alilazwa kwenye hospitali ya Kiwandani na kuwa baadaye macho 
yake yalianza kubadilika na kuwa ya njano.
 ''Tulifanya booking ya
 ndege kuelekea Bugando, tulichelewa, tukapata jana amefikishwa Bugando 
leo asubuhi tumepata taarifa kuwa amefariki dunia'' anafahamisha Kocha 
Mexime.
 Hata hivyo anasema kuwa  hadi sasa wapo katika taharuki 
wachezaji wote wanalia, watajaribu kuomba shirikisho la soka liahirishe 
mechi zake za karibuni hadi hapo watakapomaliza mazishi ya mchezaji 
mwenzao.
 Nimemfahamu David Burhan akiwa timu ya Prison wakati ule
 akiwa chini ya kocha Juma Mwambusi, baadaye Mwambusi alipohamia Mbeya 
City naye David Burhani akahamia timu hiyo nadhani kutokana na kocha 
huyo kutambua umuhimu wa golikipa huyo kwa timu yake mpya.
 Chini 
ya golikipa David Burhan timu hiyo ilifanikiwa kufanya vyema katika ligi
 hiyo mwaka 2013-14 kiasi cha kushika nafasi ya nne katika ligi hiyo.
 Burhani aliondoka katika timu ya Mbeya City na kujiunga na timu ya Kagera Suger hadi kifo kilipomchukua.
 Inna Lillahi Waina Ilayhi Rajiuwna!!!!




game slot
ReplyDeletegame slot gacor
game slot terbaik
game slot terpercaya
games slot gacor
link slot gacor terpercaya
link slot gacor
link slot
main slot
online slot