|  | 
| 
MADIWANI 24 wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma 
wanafanya ziara ya siku nne wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya kwa nia ya 
kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo,utoaji huduma za kiafya CHF,Masjala 
ya ardhi na mafanikio ya ukusanyaji wa kodi kwa ngazi za vijiji, mitaa 
na wilaya. 
 
Akizungumza
 kwa njia ya simu juu ya ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri 
ya Namtumbo Bw. Mussa Zungiza(pichani juu) alisema kuwa ziara hiyo itaongozwa na 
Mwenyekiti wa Halmashauri Bw. Stephan Nana ambayo italenga kujifunza 
mafanikio mbalimbali ambayo halmashauri ya wilaya Mbozi imeyapata 
kutokana na kujali utawala bora kati ya wananchi na watendaji wa 
serikali. 
 
Bw. Zungiza alisema kuwa halmashauri 
ya wilaya ya Namtumbo ina fursa nyingi za kiuchumi
 zikiwemo zile zitokanazo na mazao ya biashara na chakula kama vile 
Tumbaku,Korosho,Ufuta, Alizeti na mazao ya chakula ambayo ni mahindi na 
mpunga ambayo iwapo wananchi wakiyatumia vyema wanaweza kujikwamua 
kiuchumi na kuondokana na umaskini. 
 | 
|  | 
| Mkurugenzi Mtendaji wa Halmaashauri ya Wilaya ya Mbozi Levison Chillewa | 
|  |  |  | 
|  |  | ''Wilaya
 hizi zinafanana kwa kila hali kuanzia mazao yanayolimwa. jiografia 
yake... ni muhimu kujua mbinu mbadala za uzoefu ili kuboresha huduma za 
kijamii na kiuchumi ndani ya halmashauri yetu,''alisema. 
 
 
 ''Tumezingatia
 mafanikio ya Mbozi katika maeneo mengi  
..kama vile ukusanyaji kodi kwa 
ngazi za vijiji, kata na wilaya, uundwaji wa miji midogo, hati miliki za
 kimila ambazo wananchi wanakopesheka kutokana na ardhi yao ya 
asili,''alisema Bw. Zungiza. 
 
Alifafanua kuwa 
Wilaya ya Mbozi imefanikiwa katika usimamizi wa miradi kutoka ngazi za 
kata na vijiji jambo ambalo linaonesha kuna ushirikishwaji mkubwa baina 
ya watendaji wa serikali na wananchi. 
 
Bw. 
Zungiza alisema kuwa ziara hiyo inaanza leo na kukamilika Januari 20 
ambapo ambapo pia madiwani hao watapata fursa ya kutembelea wilaya ya 
Njombe iliyoko mkoani Iringa ambakoina mandhari na jiografia
 inayoshabihiana na wilaya ya Namtumbo. 
 
 ''Wilaya
 hizi zinafanana kwa kila hali kuanzia mazao yanayolimwa. jiografia 
yake... ni muhimu kujua mbinu mbadala za uzoefu ili kuboresha huduma za 
kijamii na kiuchumi ndani ya halmashauri yetu,''alisema.  
 | 
 Kwa
 upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Bw.Levison 
Chilewa alisema kuwa, mafanikio ya Halmashauri hiyo yanatokana na 
ushirikishwaji uliopo baina ya watendaji wa serikali na wananchi ambapo 
hamasa kubwa imetokana na wananchi kukubali kuhudhuria mikutano ya 
vijiji na kata na kwamba viongozi wa serikali wamehimizwa kuwa na 
utaratibu wa usomaji wa mapato na matumizi kwa wananchi.
 
Post a Comment