| 
 
MCHUANO
 wa ligi kuu umeendelea leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine 
Jijini ambapo wenyeji Mbeya City waliwakaribisha Coastal Union ya Tanga 
na kuilazimisha kutoka sare ya bao 1-1. 
 
Mchezo
 huo umeanza kwa kuviaziana ambapo timu ya Coastal Union ndiyo ilikuwa 
ya kwanza kuliona lango la timu ya Mbeya City dakika
 ya saba ya mchezo baada ya mchezaji wa timu ya Coastal Union Haruna 
Moshi Boban kuwatoka walinzi wa Mbeya City, Anton Matogolo,Alex Seth na 
Steven Mazanda  na kujipatia bao kwa mkwaju hafifu uliompita golikipa wa
 timu ya Mbeya City David Baruani. 
 
Goli
 hilo liliamsha hoihoi kwa washabiki wachache wa timu ya Coastal Union 
ambao walikuwa wakiburudisha uwanja kwa ngoma yao ya Mdumange. 
 
Baada
 ya goli hilo wachezaji wa timu ya Coastal Union walionesha kupoteza 
muda ambapo kila mpira ulipofika katika goli lao golikipa wa timu hiyo 
Hassan Shaaban alikuwa akiuchezea chezea kwa muda mrefu bila kuupiga 
hali ambayo iliibua malalamiko kwa washabiki ambao walianza kumzomea. 
 
Hadi
 kipindi cha kwanza kinamalizika Coastal Union walitoka kifua mbele kwa 
bao 1-0,ambapo hata hivyo Golikipa wa Coastal Union Shaaban alitoka nje 
ya uwanja baada ya maumivu ya musuli na badala yake kuingia Said Libawa. 
Kipindi
 cha pili kilianza kwa mashambulizi makali yaliyofanywa na timu ya Mbeya
 City na hivyo kulazimisha kona tatu zilizoelekezwa kwa timu ya Coastal 
ambazo hata hivyo hazikuzaa matunda.
 
 Mchezo huo ambao 
ulitawaliwa na kipyenga cha mara kwa mara kutoka kwa refarii Oden Mbanga
 wa Dar es salaam aliyesaidiwa na washika vibendera Hamis Chang'walu na 
Omar Kambangwa kutokana na rafu za hapa na pale.
 
 Mashambulizi 
katika lango la timu ya Coastal yalizaa matunda katika dakika za lala 
salama ambapo katika dakika ya 89 wachezaji wa timu ya Mbeya City 
walionana vizuri na kusababisha goli la kusawazishwa lililofungwa kwa 
njia ya kichwa na mchezaji wa timu ya Mbeya City Mwagane Yeya aliyeingia
 katika kipindi cha pili.
 
 Hata hivyo dakika chache baadaye 
refarii ametoa kadi nyekundu kwa wachezaji wawili wa timu ya Coastal na 
Mbeya City ambao
 walionekana kubishana uwanjani ambao ni Marcus Ndeheli na Richard Peter
 na baadaye zikiwa zimesalia sekunde kadhaa kumalizika kwa mchezo Haruna
 Moshi naye alipewa kadi nyekundu kwa kumtolea lugha ya matusi mshika 
kibendera Hamis Chang'walu.
 
 Hadi Kipyenga cha mwisho kinapulizwa timu zilikuwa sare ya bao 1-1.
 | 
Post a Comment
Post a Comment