|  | 
| Wababe wa Prison kikosi cha JKT Oljoro ambacho kiliwapeleka mchakamchaka Maafande wa Prison na kuwatandika nyumbani Bao 1-0 | 
|  | 
| Kikosi cha Prison kilichocheza na Maafande wa JKT Oljoro na kutandikwa bao 1-0 | 
|  | 
| JKT Oljoro wakifurahia bao lililopatikana dakika ya 6 ya mchezo | 
|  | 
| Hata hivyo penati hiyo iliyopigwa na mchezaji wa Prison Jeremia Juma iliokolewa na Golikipa wa timu ya JKT Oljoro Damas Kugesha. | 
|  | 
| Wachezaji wa timu ya Prison pamoja na wachezaji wa timu ya JKT wakihaha katika lango la timu ya JKT baada ya kupigwa kona ambayo haikuzaa matunda. | 
|  | 
| Hadi timu zinatoka mapumziko JKT Oljoro ilikuwa inaongoza kwa bao 1-0 | 
|  | 
|  | 
| Golikipa wa JKT Damas Kugesha alionekana kuwa na kazi nzito ya kuchomoa mikwaju ya wachezaji wa Prison. | 
|  | 
| Mara kadhaa mwamuzi Zakaria Jacob alionekana kuwa mkali kwa kuwazawadia kadi ya njano wachezaji ambao walionekana kucheza kabumbu isiyostahili | 
|  | 
| Hali haikuwa nzuri kwa timu ya Prison kutokana na wachezxaji wa JKT kuonekana kudhibiti kila eneo la uwanja kwani kKila alipokuwa mchezaji wa Prison walitokea wachezaji wawili wa JKT. | 
|  | 
| Wachezaji wa Prison mara nyingi walionekana kushindwa kulifikia goli la JKT kutokana na wachezaji hao kuwa wepesi kukimbia huku na kule na hivyo kuwapa kazi nzito maafende wa Prison. | 
|  | 
| Mbali na maelekezo kutoka kwa mwalimu wao Alex Mwamgaya wachezaji wa JKT oljoro hawakuacha kupeana mikakati kila mpira uliposimama kwa muda | 
|  | 
| Ni kama bahati mbaya kwa mwalimu wa timu ya Prison David Mwamwaja ambaye amekabidhiwa kikosi hiki muda mfupi baada ya timu hiyo kuchabangwa mabao 2-0 na wadogo zao Mbeya City juma lililopita. | 
|  | 
| Kocha wa Prison Mwamwaja akitoa utetezi wake mbele ya waandishi wa habari sababu za kushindwa kwa mechi hiyo na kuahidi kujipanga katika mechi zijazo. | 
|  | 
| Kwa upande wake mwalimu wa timu ya JKT Oljoro Alex Mwamgaya kwake ilikuwa ni furaha kutokana na ushindi ulioipata timu yake. | 
|  | 
| Kilio cha mashabiki wa timu ya Prison ni kuutaka uongozi ukabidhi timu kwa wananchi kama wanavyoonekana pichani. | 























Post a Comment