MAPATO
 kwa mechi ya ligi ya Vodacom kati ya timu za Mbeya City ya Jijini Mbeya
 na Simba ya Jijini Dar es salaam yamevunja rekodi ya michezo yote 
iliyowahi kuchezwa nje ya Jiji la Dar es salaam kwa kuingiza kiasi cha 
sh. milioni 105.
Mechi
 iliyowahi kuingiza kiasi kikubwa cha mapato katika uwanja huo ni ile 
iliyochezwa kati ya Timu ya Mbeya City na Yanga ya Dar es salaam katika 
uwanja huo mwaka jana na kuingiza kiasi cha sh. milioni 100.
Katika
 mechi hiyo ya jana ambayo timu hizo zilitoka sare ya goli 
1-1,jumla ya tiketi 21,000 ziliuzwa ambapo tiketi moja iliuzwa kwa 
sh.5,000 hata hivyo tiketi hizo ziliisha mapema na kusababisha baadhi ya
 mashabiki waliohitaji kushuhudia mchezo huo kubaki nje ya uwanja.
Mbali
 na mashabiki waliokosa tiketi kushindwa kuingia uwanjani, mwandishi wa 
habari hizio alishuhudia umati wa mashabiki ambao walikuwa na tiketi 
mkononi kuendelea kubaki nje hadi kipindi cha kwanza kinamalizika 
kutokana na msururu mrefu wa kuingia uwanjani.
Wapenzi wa soka 
walianza kukata tiketi  majira ya saa 2:00 asubuhi na kuanza kuingia 
uwanjani saa 4:30 ambapo hata hivyo msururu  mrefu wa wapenzi 
waliohitaji kuiona mechi hiyo ilisababisha kushindwa kuingia uwanjani 
kwa wakati.
Katika
 hatua nyingine baadhi ya watu walipata fursa ya kujiongezea kipato kwa 
kununua vitabu vya tiketi za mechi hiyo na baadaye kuziuza kwa bei ya 
sh.8,000 hadi sh.10,000 badala ya bei ya kawaida iliyopangwa na TFF ya 
sh. 5,000 kwa kila tiketi.
Mbali
 na tiketi hizo kuuzwa kwa bei ya juu bado kuna baadhi ya tiketi 
zilionekana kutokidhi viwango ambapo mwandishi wa habari hizi 
alishuhudia mmoja wa wasemaji wa timu ya Mbeya City Freddy Jackson akiwa
 na tiketi zisizopigwa mhuri na kusema kuwa tiketi hizo zimeghushiwa kwa
 nia ya kuhujumu mapato ya mchezo huo.
Akizungumza
 mapato ya mchezo huo Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu mkoa wa 
Mbeya Elias Mwanjala alisema kuwa  jumla ya tiketi 21,000 ziliuzwa na 
kumalizika na kuingiza mapato jumla ya sh. milioni 105.
Katika
 mapato hayo kila timu ilipata kitita cha sh. milioni 25.3 ambapo 
sh.milioni 12.8 zilibaki kwa ajili ya uwanja,sh.milioni 7.7 kwa ajili ya
 maandalizi na sh. milioni 7.7 kwa
 ajili ya kamati ya ligi ilhali sh. milioni 3.8 zilikuwa ni kwa ajili ya
 chama cha mpira wa miguu TFF.







Post a Comment