Jambo jema linofaa lisaidie jamii,
Lijenge mustakabali,na watu walikubali,
Likubalike kwa aali,wa nyumbani na wambali,
Mjionapo si wakweli,achieni ngazi mthaminiwe.
Mfano huu ni kweli, viongozi mafisadi,
Ardhi na rasilimali,hudhulumu kwa ahadi,
Miaka mitano si mbali,wazidi fanya kusudi,
Mjionapo si wakweli achieni ngazi mthaminiwe.
Walisema wanaweza, waliweza kutuibia,
Wakajilia pweza,na nje ya nchi kukimbia,
Huku tumetelekezwa,zatushinda familia,
Mjionapo si wakweli, achieni ngazi mthaminiwe.
Watu waliwazomea, kila wapitapo,
Wakajinadi kwa mazoea,na aibu ingalipo,
Na wapo walolowea, nje ya nchi ndipo walipo,
Mjionapo si wakweli achieni ngaziz mthaminiwe.
Ujumbe huno ni wenu, viongozi mafisadi,
Mkiwacha kazi kwenu,nimenena pasi kedi,
Bali jueni ni dhima yenu,kutekeleza ahadi,
Mjionapo si wakweli, achieni ngazi mthaminiwe.
Wakatabahu
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Nimefurahi kuliona jamvi jingine. Sikuwahi lijua lakini nimekukuta kwa kaka Fadhy Mtanga. Great job Brother and keep it up.
ReplyDeleteBlessings
Asante kwa kuwapasha. Wasijidai hawasikii. Wamesikia sana.
ReplyDeleteHeri ya mwaka mpya kaka.
Heri ya Mwaka Mpya kwenu bloggers wote. Na wasomaji wetu.
ReplyDeleteBlogi poa sana, tatizo sasa umekuwa mvivuwa kuandika kaka
ReplyDelete