Nikifa msinililie sana,bali mtafakari mema yangu na kuyafanyia kazi na kujifunza kwa maovu yangu ili mpate kujifunza kwayo.
Nikifa jifunzeni kwa mapungufu yangu ili iwe ni mazingatio kwa kutoyarejea niliyoyafanya na iwe ni Ibra mazingatio kwa vizazi vijavyo.Nikifa msitafute kurithi mali zangu bali mwatakiwa kurithi busara na hekima zangu ingawa kila binadamu hakosi mapungufu ambayo anastahili kusamehewa kwayo.
Nikifa mnizike haraka ili nisioze nikawatia kero na kunitema mate, hakuna awezaye kunirejesha hata mkilia sana amali zangu nilizozitanguliza akhera ndiyo kinga yangu mujarabu inayoweza kuniokoa na adhabu ya kaburi.
Nikifa nifanyieni mema kwa kuitunza familia yangu,ifarijike wajione kama wako na baba yao.Walionikebehi hawatoniona tena na hata wakinisema siwezi kuwasikia na wala haitowasaidia kitu kwani kila mmoja yu njiani kuelekea nielekeako mimi.
Nikifa mnizike kuelekea kibla wala msichague ni wapi pafaa kunizika kwani makadirio ya maisha yangu ni pale nifiapo na ndipo ninapostahili kuzikwa, msikose kunifanyia mambo muhimu kwa mila na desturi za dini yangu.
Nikifa wala msihangaike kutafuta sababu za kifo changu mkakamata wachawi na vinginevyo, bali mnapaswa kujua kuwa kila kiumbe lazima kitauonja umauti, na kila mja amekadiriwa riziki yake itapatikana na mwisho wake na hata mahala pa kufia amepangiwa na aina ya kifo .
Wakatabahu
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Muhimu tuhuzunike, la sivyo usitutoke,
ReplyDeleteIli chozi situtoke, labda usiondoke,
Ili tusihuzunike.
Ikibidi ututoke, muhimu tuhuzunike,
Kote tukakusanyike, kidini tukakuzike,
Machozi yatudondoke.
Kulia ni lazima kwani si mtu kama watu wote
ReplyDelete