Ads (728x90)




WABABE wa Yanga timu ya wakata Miwa Mtibwa ya Morogoro leo imegonga mwamba baada ya kupelekeshwa puta na timu ya maafande wa Prison ya Mbeya na kulazimishwa kutoka suluhu ya bila kufungana katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Mpira huo ulianza kwa kasi kwa kila mmoja kuliandama lango la mwenzie ambapo kinyume na miaka ya nyuma timu ya Prison imeonekana kushindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani kwa kulazimisha kutoka suluhu kwa mechi za nyumbani.

Hadi mapumziko timu hizo zilizokuwa zinachezeshwa na refarii Hashimu Abdallah kutoka Jijini Dar es salaam zilikuwa zilikuwa hazijaweza kuona goli la mpinzani wake.

Mbali na michomo kadhaa iliyokuwa ikielekezwa katika lango la Mtibwa na kuokolewa nma golikipa Shaaban Kado, Prison nao walikuwa wakihaha kujaribu kuokoa michomo iliyokuwa ikilengwa kwa golikipa wake Daud Abdalla ambaye kwa muda mwingi alikuwa akihaha golini akiwapanga walinzi wake Henry Mwalugala, Laurian Mpalile, Lugano Mwangama na David Mwantika.





Uwanja huo mbali na kuhudhuriwa na watu wachache ukilinganisha na mechi ya Yanga na Prison ambayo nayo timu hizo zilitoka suluhu, ulipambwa na mashabiki waliojaribu kuleta vionjo vya kejeli za kimichez.o


Post a Comment