| WABABE wa Yanga timu ya wakata Miwa Mtibwa ya Morogoro leo imegonga 
mwamba baada ya kupelekeshwa puta na timu ya maafande wa Prison ya Mbeya
 na kulazimishwa kutoka suluhu ya bila kufungana katika uwanja wa 
Sokoine jijini Mbeya. 
 Mpira huo ulianza kwa kasi kwa 
kila mmoja kuliandama lango la mwenzie ambapo kinyume na miaka ya nyuma 
timu ya Prison imeonekana kushindwa kuutumia vyema uwanja wake wa 
nyumbani kwa kulazimisha kutoka suluhu kwa mechi za nyumbani.
 
 Hadi
 mapumziko timu hizo zilizokuwa zinachezeshwa na refarii Hashimu 
Abdallah kutoka Jijini Dar es salaam zilikuwa zilikuwa hazijaweza kuona 
goli la mpinzani wake.
 
 Mbali na michomo kadhaa 
iliyokuwa ikielekezwa katika lango la Mtibwa na kuokolewa nma golikipa 
Shaaban Kado, Prison nao walikuwa wakihaha kujaribu kuokoa michomo 
iliyokuwa ikilengwa kwa golikipa wake Daud Abdalla ambaye kwa muda 
mwingi alikuwa akihaha golini akiwapanga walinzi wake Henry Mwalugala, 
Laurian Mpalile, Lugano Mwangama na David Mwantika.
 | 
Post a Comment