Ads (728x90)

Wapo walosimama na kjiona kama wako hima, bali waishi kwa kutetema na kujawa nma dhulma, iwapi yao nia njema ilhali dunia si njema na wala si mahala pema?

Nia ni njema bali matumaini si mema, walao hula wima bila kunawa tena kwa kukomba nakusaza makombo kwa yatima ambao hudiriki mlo mmoja wa chakula kiso chema.

Hula kwa kujaza matumbo na kutafakari maisha magumu na machungu, siku hizo zenda mbele na katu hazirudi nyuma.

Wako wapi watu wema waliotajwa kwa majina na utukufu wakatukuta nasi tukawawekea kumbukizi njema?

Wako wapi wafalme walikokula wao na kuwaacha vijakazi wakila makombo na matumbo kuwauma?

Wako wapi wajane wahanga ambao waume zao wamehajiri ama kuuliwa bila sababu za kina na kuziacha familia roho zao zinauma?

Wawapi hao watwana walotawala kwa mabavu na kudiriki kubaka vigori vilo ndani kisa hamasa za kisiasa ilhali nasi macho yetu yanaona?

Tupige mbiu kukataza maovu na waovu watokomee ili nia iwe ni kuongozwa na watu wema.

Wakatabahu

Post a Comment