Ujumbe mzito wa Bill & Melinda Gates Foundation kutoka 
Marekani ukiongozwa na Senior Programme Officer (Market Access) Richard 
Rodgers ulitua leo kwa ndege ya kukodi kwenye ofisi za Kapunga Rice, 
Chimala na kufanya mazungumzo na George Mtenda wa Mtenda Kyela Rice 
Supply Company ya Mbeya.
Rodgers
 alifuatana na Karen Harkono na Niraj Varia na kwa upande wa Mtenda 
Kyela Rice wawakilishi walikuwa Emile Malinza, Josiah Nyato na Jesko 
Linga.
Gates Foundation 
waliridhika na maelezo yakinifu kutoka Mtenda Kyela Rice na wameahidi 
kusaidia katika nyanja za mafunzo kwa wakulima na upatikanaji wa 
pembejeo za
 kilimo.
Mazungumzo kati
 ya pande hizo mbili yanaendelea na mwelekeo
 utapatikana baada ya miezi minne kuanzia sasa kwani Rodgers ameahidi 
kuwasiliana na ofisi zao za Marekani na kuwapa mrejesho wa ziara yake.
Post a Comment
Post a Comment