| 
JUMUIYA ya Waislamu wa Ahmadiya
  nchini imesema kuwa sababu za machafuko katika nchi za Mashariki ya Kati
  ambako asilimia kubwa ni waislamu zimetokana na waislamu kutofuata kwa
  vitendo muongozo wa Koran Tukufu na Hadithi sahihi za Mtume Muhammad (SAW). 
 
Kauli hiyo imetolewa na kiongozi
  mkuu wa Jumuiya ya Ahmadiya nchini Amir Tahir Mahmood Chaundry mara
  alipowasili Jijini Mbeya kwa ajili ya ziara ya Mkutano wa Amani inayofanyika
  Jijini hapa. 
 
Amir Chaundry alisema kuwa mchango
  wa Uislamu katika amani ya nchi na dunia ni mkubwa na kwamba machafuko
  yanayoendelea katika nchi nyingi zenye waislamu wengi zinatyyokana na
  waislamu wenyewe kutofuata maagizo yanayofundishwa katika Kitabu kitukufu cha
  Koran.   
 
Akijibu swali kuhusu wajibu wa
  Jumuiya hiyo katika kusimamia amani duniani ilhali nchi nyingi za kiislamu
  zina machafuko, Kiongozi huyo wa ngazi ya juu katika Jumuiya ya Ahmadiya
  nchini alisema, wajibu wa waislamu ni kutii sheria na kufuata maamrisho ya
  Mwenyezi Mungu na Mtume wake. 
 
Alibainisha kwa kusema kuwa hali
  inayotokea katika nchi nyingi ikiwemo nchi aliyotokea ya Afghanistan
  imetokana na kuwepo kwa waislamu wasiojua vyema uislamu. 
 
Alisema kuwa waislamu wengi wako
  kwa majina lakini hawatekelezi Uislamu kama unavyoagizwa na Mwenyezi Mungu na
  kuwa Jumuiya ya Ahmadiya kwa nafasi yake imejitahidi kutangaza amani na
  utulivu duniani kote kwa njia za midahalo,makongamano ya kidini, mikutano na
  kusambaza vipeperushi. 
 
Akinukuu baadhi ya aya za Koran
  Amir Chaundry  alisema kuwa Jumuiya ya Ahmadiya inaamini kuwa kila mtu
  ana uhuru wa kuabudu mahala atakako bila kushurutishwa  na mtu yoyote.  
 
''Utaona katika nchi za Kiislamu,
  Waislamu kwa waislamu wanauana wenyewe kwa wenyewe, hawa ni waislamu lakini
  hawaujui Uislamu, tukiusoma vyema Uislamu hakuna vurugu inayoweza
  kutokea,''alisema Amir Chandry. 
 
 | 
Post a Comment