La Dodoma azimio, Makene limetulia,
Lafaa kuwa zingatio,Bloguni kutumia,
Tena liwe karipio, watakao vurugia,
Azimio la Dodoma,liwe la wanaBlogu.
Kwa uhuru twandikia, wengi wanatusomea,
Maadili kupindia, hako wa kutukemea,
Uhuru tunotumia, sote twaushere’kea,
Azimio la Dodoma,liwe la wanaBlogu.
Sheria kuiwekea, madhara kutukingia,
Uhuru uliopea,majina twajiandikia,
Msaliti kitokea,Blogu tutakimbia,
Azimio la Dodoma, liwe la wanaBlogu.
Wazo lenu wa Dodoma,mkono naliungia,
Kikao chenu ni dhima,ni mfano kuigia,
Fikira hazitokoma,wanaBlogu kuchangia,
Azimio la Dodoma, liwe la wanaBlogu.
Miruko,Kazonta,Mtangoo,jema mlofikiria,
Msaki, Msangi katika mtandao, wote wanalichangia,
Nyembo,Ndesanjo,na wengineo,hima wanaliwania,
Azimio la Dodoma, liwe la wanaBlogu.
Adabu kuzingatia, katika kuandikia,
Maadili kufatia, ya uandishi Blogia,
Wasomao jifunzia,kazi zilizotulia,
Azimio la Dodoma, liwe la wanaBlogu.
Wakatabahu kuungia,beti saba natulia,
Hima sote kubalia,la Dodoma liwe njia,
Kwamba si nadharia, kwa vitendo fuatilia,
Azimio la Dodoma,liwe la wanaBlogu.
Ndimi Mkwinda Rashid, kalamu naiachia,
Kamwe sina ukaidi,kwa hili kuliungia,
Nitafanya tashdidi, wengi kuwashawishia,
Azimio la Dodoma, Liwe la wanaBlogu.
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mkwinda mashairi yako huwa yanarejesha haraka ile tamu ya ushairi niliyowahi kuwa nayo shuleni. Wengine wanaweza kuwa hawakioni haraka. Vina na mizani yako siyo ya kulazimisha. Yachuruzika yenyewe kwa raha tele ya kusoma ama kughani. Rambirambi zikufikie.
ReplyDeleteKwa nini nisibaini, huu mwana mwenye heshima?
ReplyDeleteKwa huu wako ugani, kukiunda chetu chama
Sina lakuongezani, mkuki umeshachoma
Azimio na lidumu, mabaradhuli uani