Mambo vipi washikaji, mngali mpo katika vitundu vyenu ama mmeamka kutafakari ya dunia, yale yawatafunayo na yale muyatafunayo, mkitafuna jueni iko siku yatawatafuna, kuleni kwa wasaaa, bali msilewe mkila mkakosa mustakabali hata wa kuziongoza kumudu utashi katika familia zenu seuze kuwa na mamlaka ya kuongoza jamii ya watu wanaokaribia milioni 40.
Ni hatari lakini ni salama kila siku ni usanii na sanaa ambazo hazina matokeo mujarabu kwa walala hoi na wale walala hai, hayo ndiyo maisha ya kila siku watu wanaotarajia maisha bora, huku wengine wakila na kusaza tena hula bila hata kunawa mikono, ni aibu tupu, ni nani atakaye ibuikua kuokoa jamii hii ya Wadanganyika huku kila siku zinabuniwa mbinu mbadala za wizi wa kula na kura.
Ni aibu hii kwa wadanganyika waliojifunika blanketi gubigubi na kujivika miwani ya mbao Mintaarafu wasione kilicho mbele yao, na kusahau kilichojiri kabla ya kufikia siku waliyonayo hivi sasa, ni usanii na ni hatari kutumika ili kuwanufaisha wachache wanaoamua kujishibisha matumbo yao, hawaoni hata dhambi kwa Mwenyezi Mungu kufanya mambo haya ya aibu LOOOO!!!!! , Mungu ona udhalili huu na ikiwezekana toa adhabu inayostahili kulingana na matendo yao hapa hapa duniani.
Wakatabahu
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment