Hayati Mwalimu Julius Nyerere akiwa na Waziri mkuu wa enzi hizo Hayati Rashid Mfaume Kawawa katika harakati mbalimbali za Uhuru wa nchi yetu.
Hayati Edward Moringe Sokoine atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wa kupingana na rushwa, ufisadi na hujuma dhidi ya mali za umma.
Jaji Joseph Sinde Warioba ni miongoni mwa watu wanaopaswa kuenziwa katika mchango wa nchi yetu kwa miaka 50 iliyopita.
Dkt. Salim Ahmed Salim, heshima yake inaendelea kutukuka ndani na nje ya nchi yetu, wananchi bado wanaheshimu fikra zake katika kupigania harakati za ukombozi na usuluhishi miongoni mwa nchi za Kiafrika.
Edward Lowasa Pamoja na kujiuzulu wadhifa wa Uwaziri mkuu kwa kipindi kifupi cha uongozi wa awamu ya nne anatajwa kuwa ni miongoni mwa viongozi mahiri walioamua kujitoa mhanga kwa ajili ya kulinda heshima ya serikali iliyopo madarakani na chama kinachotawala,Anaendelea kuandamwa kwa kashfa ya ufisadi kutokana na kitendo chake cha kujiuzulu wadhifa wa Uwaziri mkuu,huku tuhuma hizo zikimjengea heshima miongoni mwa wananchi na hata kuwa tishio ndani ya chama kuelekea uchaguzi mkuu 2015.
Fredrick Sumaye anatajwa kuwa ni miongoni mwa mawaziri walioitumikia nchi na kupiga hatua z amaendeleo kwa kipindi cha miaka mitano cha utawala wa awamu ya tatu ya uongozi wa nchi yetu.
John Malecela, mchango wake unaheshimiwa zaidi ndani ya chama na amekuwa miongoni mwa hazina zinazolindwa na chama tawala pamoja na kuwa nje ya uongozi na ulingo wa kisiasa.
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment