Nadhani tukio la hivi karibuni la Mwana wa 'Kukaya'Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 'JK' kulizungumzia suala la filamu ya Darwins Nightmare ya Bw. Hubert Sauper limechukua na kuhamisha fikra za wadanganyika.
Mimi nadhani watunzi wa riwaya na tamthiliya tutakuwa katika wakati mgumu kwa kuzuiwa kutoa kazi za kisanii na kifasihi kwa kuhofia dhana ya kuvuka mipaka ya fikra kwa matukio halisi yaliyopo.
Inakuwa ngumu kuchangia suala hili kabla ya kuiona filamu hiyo lakini kikubwa ni kwamba utunzi wa tamthiliya ni ubunifu wa kisanii uliochagizwa na fikra binafsi za mtunzi kwa mnasaba wa matukio halisi yanayojiri katika jamii.
Hebu wanablogi waliobahatika kuiona filamu hiyo watudadavulie yaliyomo ndani ya filamu hiyo ili tuanze kuchanganua kilichopo tujue pumba zipi na mchele upi, naamini,akina Sultani Tamba na wengine waliomo ndani ya Blogi wataungana nami kulichangia hili.
Wakatabahu
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mjadala huu, hotuba ile na yanayoendelea kwa wakati huu, ni ishara ya wazi kuwa kuna tatizo mahali, ama kwa uongozi, mitizamo, mapokeo ya changamoto au mahali fulani, lakini kwa ujumla yote yanayojiri ni ishara za mapungfu mahali fulani.
ReplyDelete