Ads (728x90)


James Mwampondele (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanahabari baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu Uchumi na Fedha wa CCM mkoa wa Mbeya.



Mwandishi wa habari na mwkilishi wa gazeti la Chama (UHURU) mkoa wa Mbeya Solomon Mwansele akimpongeza kwa kwa kuchaguliwa kuwa  Katibu Uchumi na Fedha mkoa wa Mbeya James Mwampondele






MJASIRIAMALI na mwekezaji Jijini Mbeya James Mwampondele(50) ameshinda nafasi ya Katibu Uchumi na Fedha ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoani Mbeya kwa kupata jumla ya kura 36 kati ya kura 65 za wajumbe wote wa uchaguzi huo.
Mwampondele aliwabwaga wapinzani wake aliochuana nao  vikali katika uchaguzi huo ambao ni  Steven Mwakajumilo aliyepata kura 25  na Mshereheshaji mashuhuri Jijini Mbeya Charles Mwakipesile aliyepata kura 4.
Wagombea Mwakajumilo na Mwakipesile waliwahi kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu kuwania nafasi ya Ubunge na kushindwa kwenye mchujo wa ndani wa CCM ambapo Mwakipesile aliwania Jimbo la Mbeya mjini na Mwakajumilo aliwania jimbo la Busokelo.
Nafasi hiyo iliachwa wazi baada ya aliyekuwa  Katibu Uchumi na Fedha wa mkoa wa Mbeya Hans Mwakisyala kufariki dunia kabla ya kumaliza muda wake uliotarajiwa kumalizika Julai mwaka huu.
Mwakisyala alipokea kijiti kutoka kwa Kenneth Ndingo aliyedumu katika nafasi hiyo kwa jumla ya miaka 15 hadi mwaka 2014 alipoamua  kupumzika.
Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa nafasi hiyo Mwampondele aliwashukuru wanachama wa CCM kwa kumuunga mkono na kuahidi kuendeleza mazuri ya mtangulizi wake  ambapo pia aliomba ushirikiano wa hali na mali kwa viongozi wa chama.
‘’Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu, pili nawashukuru wana CCM wote pamoja na viongozi wangu bila kuwasahau wagombea wenzangu, naahidi kushirikiana nanyi kwa hali na mali katika kusimamia sera na ilani za chama chetu kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi,’’alisema Mwampondele.

Post a Comment