Ads (728x90)

Watoto hawa wakazi wa Mabatini Jijini Mbeya wakicheza katika mto nyakato za masomo wenzao wakiwa madarasani bila kujali kuwa kufanya hivyo kunachangia kudorora kwa uelewa wao na hata kuhatarisha afya zao kwa kupata magonjwa ya milipuko kutokana na maji ya mto huo kutumika kwa matumizi mbalimbali katika maeneo hayo.Ipo haja kwa familia kufuatilia nyendo za watoto wao mashuleni badala ya kuwaachia mzigo huo walimu pekee kwani athari inayoweza kutokea kwa mchezo wa aina hii unaweza kugharimu afya za watoto hawa mbali na kudorora kwa kiwango chao cha elimu.

Post a Comment