| 
 
Mpambano
  kati ya timu mbili za ligi kuu Yanga ya Dar es salaam na Mbeya City ya Mbeya
  umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.Mchezo huo ambao ulitawaliwa
  na shamrashamra na hoihoi uwanja mzima ulikuwa ni wa vuta nikuvute ambapo
  hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimetoka uwanjani suluhu bila ya kufungana. 
Kipindi
  cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikitaka kupata bao la kuongoza,
  bahati iliwaangukia timua Mbeya City mnamo dakika ya 45 ambapo mchezaji
  Mwagane Yeya alitumia udhaifu wa walinzi wa timu ya Yanga na kufanikiwa
  kuipatia timu yake bao ambalo lilifungwa kwa kichwa na kumuacha golikipa wa
  timu ya Yanga Ali Mustafa Baltez akigaa gaa pembeni huku mpira ukiwa umetinga
  wavuni. 
Mara
  baada ya bao hilo la Mbeya City Yanga ilianza kulishambulia lango la Mbeya
  City kwa kasi kubwa na kusababisha dakika ya 65 golikipa wa timu Mbeya City
  kuutema mpira ambapo mshambuliaji wa Yanga Jerry Tegete aliusukumia wavuni
  lakini goli hilo lilikataliwa na mwamuzi  Andrew Shamba. 
Mnamo
  dakika ya 71 Yanga ilifanikiwa kupata bao la kusawazisha kupitia mchezaji
  Didier Kavumbagu ambaye aliwatoka walinzi wa timu ya Mbeya City na
  kutumbukiza bao kimiani,hadi kipyenga kinapulizwa mabao yalikuwa sare ya 1-1. 
Awali
  mchezo huo ulitawaliwa na vituko na vurugu za hapa na pale ambapo kabla ya
  mechi hiyo kuanza wakati wachezaji wa timu ya Yanga wanaingia uwanjani na
  Basi lao kundi la mashabiki wa timu ya Mbeya City walianza kuvurumisha mawe
  na chupa na kusababisha Basi hilo kuvunjwa kioo cha upande wa dereva Maulid
  Kiula na kumjeruhi mkono wake wa kulia. 
Aidha
  kituko kingine kilichotokea kabla ya mchezo huo kuanza ni kukutwa mayai
  matatu yaliyochorwachorwa katikati ya uwanja ambapo Meneja wa uwanja huo
  Modestus Mwaruka aliyaondoa na kuyapeleka ofisini. | 
soka katika mazingira haya haliwezi kutupeleka mbali.Tujirekebishe
ReplyDelete