Ads (728x90)




 Bloga Wetu Dodoma
ZIKIWA zimebaki dakika 345,600 sawa na saa 5,760 ambazo ni takribani siku 240 Rais Jakaya Kikwete jana amefanya mabadiliko mengine ya Wakuu wa wilaya kwa kuwatupa nje ya ulingo wakuu wa  Wilaya 12 na kuteua sura mpya 27.

Uteuzi huo wa Rais Kikwete umekuja huku kukiwa na tetesi za baadhi ya wakuu wa wilaya waliotemwa kupangiwa kazi nyingine ikiwemo kuimarisha chama kuelekea uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

‘’Hakukuwa na sababu ya kujiingiza gharama za kulipa wakuu wa wilaya watakaostaafu na kuachishwa kazi, wakati tunakabiliwa na jukumu kubwa la zoezi la uandikishaji vitambulisho vya kupigia kura na maandalizi mengine ya uchaguzi,JK alipaswa kuwaonea huruma wananchi wake,’’alisema mkazi wa mjini Dodoma aliyejitambulisha kwa jina moja la Mazengo.

Mazengo alisema kuwa kitendo hicho ni kuiingiza serikali gharama mpya ambayo haikupaswa kutokana na vipaumbele vilivyopo kwa mwaka huu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba. 

''Mahitaji yetu si kuwa na sura mpya za wakuu wa wilaya.. kimantiki hawa wapo kisiasa zaidi badala ya utendaji, wangebadilishwa watendaji huenda tungepata ladha ya kuwepo kwa mabadiliko haya,kwanini mabadiliko yafanyike ikiwa imebaki miezi nane JK amalize awamu yake? alihoji Mazengo ambaye kitaaluma anadai ni Mwalimu.

Katika uteuzi huo wa Rais ambao umefanywa kwa niaba yake na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, JK amewapiga chini wakuu wa wilaya 12 kutokana na sababu zilizoelezwa kuwa ni umri, afya na kuimarisha utendaji wa kazi serikalini.

Waziri Pinda  aliwataja waliotenguliwa kuwa ni pamoja na James Millya aliyekuwa Mkuu we wilaya ya Longido,Elias Lali aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Ngorongoro,Alfred Msovella aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kongwa ,Danny Makanga aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Kasulu,Fatma Kimario aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe.

Wengine waliotenguliwa  ni Evarist Kalalu aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Mufindi,Abihudi Saideya aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Momba Elibariki Kingu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Igunga,Dk.Leticia Warioba aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Iringa Martha Umbulla aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kiteto,Khalid Mandia aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Babati na Elias Goroi.

Katika uteuzi huo wakuu wa wilaya 27 wameula ambao ni pamoja na Mtangazaji maarufu wa TBC Shaaban Kissu,(Kondoa)Mariam Mtima (Ruangwa),Dk.Jasmine Tiisike (Mpwapwa),Pololeti Mgema (Nachingwea),Fadhili Nkurlu (Misenyi),Felix Lyaniva (Rorya),Fredrick Mwakalebela (Wanging'ombe) na Zainabu Mbussi (Rungwe) .

Francis Mwonga(Bahi),Kiming'ombe Nzoka (Kiteto),Husna Msangi (Handeni),Emmanuel Uhaula (Tandahimba),Mboni Mhita  (Mufindi),Hashim Mgandilwa (Ngorongoro) ,Mariam Juma (Lushoto),Thea Ntara (Kyela) na Ahmad Nammohe (Mbozi)

Wengine ni aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi katika baadhi ya mikoa hapa nchini Zelothe Steven (Musoma),Pili Moshi (Kwimba),Mahmoud Kambona (Simanjiro) ,Glorius Luoga (Tarime),Zainabu Telack (Sengerema),Benard Nduta (Masasi),Zuhura Ally (Uyui) ,Paul Makonda (Kinondoni),Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na Maftah Mohamed (Serengeti).

Aidha Waziri Pinda aliwataja wakuu wa wilaya 64 waliobadilishwa vituo vyao vya kazi kuwa ni  pamoja na Nyerembe Munasa (Arumeru hadi Mbeya), Jordan Rugimbana (Kinondoni hadi Morogoro), Fatma Salum Ally kutoka (Chamwino hadi Mtwara), Lephy Gembe(Dodoma hadi Kilombero) na Christopher Kangoye (Mpwapwa hadi Arusha).

Wengine ni Omar Kwaang’(Kondoa- Karatu), Francis Mtinga (Chemba-Muleba), Elizabeth Mkwasa (Bahi-Dodoma), Agnes Hokororo (Ruangwa –Namtumbo), Regina Chonjo kutoka (Nachingwea hadi Pangani), Husna Mwilima (Mbogwe- Arumeru na Gerald Guninita  (Kilolo – Kasulu).
Wengine waliobadilishwa vituo vya kazi ni Zipora Pangani  (Bukoba hadi Igunga), Kanali Issa Njiku  (Misenyi hadi Mlele), Richard Mbeho (Biharamuro hadi Momba), Lembris Kipuyo (Muleba hadi  Rombo), Ramadhani Maneno (Kigoma kwenda Chemba), Venance Mwamoto (Kibondo kwenda Kaliua), Gishuli Charles (Buhigwe kwenda Ikungi), Novatus Makunga (Hai kwenda Moshi) na Anatory Choya kutoka (Mbulu kwenda Ludewa).

Wengine ni Christine Mndeme (Hanang’ kwenda Ulanga), Jackson Msome (Musoma kwenda Bukoba, John Henjewele (Tarime kwenda Kilosa), Dk Norman Sigalla (Mbeya kwenda Songea), Dk Michael Kadeghe(Mbozi kwenda Mbulu), Cripin Meela (Rungwe kwenda Babati) na Magreth Malenga (Kyela kwenda Nyasa).

Aliwataja wengine kuwa ni Said Amanzi  (Morogoro kwenda Singida),Antony Mtaka (Mvomero kwenda Hai), Elias Tarimo (Kilosa kwenda Biharamulo), Francis Miti(Ulanga kwenda Hanang),  Hassan Masala(Kilombero kwenda Kibondo), Angelina Mabula (Butiama kwenda Iringa), Farida Mgomi (Masasi kwenda Chamwino), Wilman Ndile  (Mtwara kwenda Kalambo).

Pia aliwataja Ponsian Nyami (Tandahimba kwenda Bariadi),Mariam Lugaila (Misungwi kwenda Mbogwe), Mary Onesmo (Ukerewe kwenda Buhigwe), Karen Yunus  (Sengerema kwenda Magu), Josephine Matiro  (Makete kwenda Shinyanga), Joseph Mkirikiti (Songea kwenda Ukerewe), Abdula Lutavi  (Namtumbo kwenda Tanga), Ernest Kahindi (Nyasa kwenda Longido), Anna Nyamubi  (Shinyanga kwenda Butiama) na Rosemary Kirigini (Meatu kwenda Maswa).

Abdalla Ali Kihato (Maswa kwenda Mkuranga), Erasto Sima (Bariadi kwenda Meatu), Queen Mulozi(Singida kwenda Ulambo), Yahaya Nawanda kutoka Iramba kwenda Lindi, Manju Msambya (Ikungi kwenda Ilemela), Xaveli Maketta  (Kaliua kwenda Kigoma), Bituni Msangi (Nzega kwenda Kongwa) na Lucy Mayenga kutoka Uyui kwenda Iramba.

Majid Mwanga amebadilishwa kituo chake kutoka (Lushoto kwenda Bagamoyo), Muhingo Rweyemamu (Handeni kwenda Makete), Hafsa Mtasiwa (Pangani kwenda Korogwe), Dk Nassor Ali Hamid (Lindi kwenda Mafia), Festo Kiswaga(Nanyumbu kwenda Mvomero), Sauda Mtondoo(Mafia kwenda Nanyumbu), Seleman Mzee (Kwimba kwenda Kilolo), Esterina Kilasi (Wanging’ombe kwenda Muheza), Subira Mgalu(Muheza kwenda Karagwe) na Jacqueline Liana (Magu kwenda Nzega).

Pia aliwataja wakuu wa wilaya 42 waliobakishwa kwenye vituo vyao vya kazi kuwa ni Jowika Kasunga (Monduli), Raymond Mushi (Ilala), Sophia Mjema (Temeke), Amani Mwenegoha (Bukombe), Ibrahimu Marwa (Nywang’wale), Rodrick Mpogolo (Chato) Manzie Mangochie (Geita), Darry Rwegasira (Karagwe), Luteni Kanali Bnedict Kitenga (Kyerwa) na Constatine Kanyasu (Ngara).

Wengine ni Paza Mwamlima (Mpanda), Peter Kiroya (Kakonko), Hadija Nyembo (Uvinza), Dk Charles Mlingwa (Siha), Shaibu Ndemanga (Mwanga), Herman Kapufi (Same), Ephraimu Mbaga (Liwale), Abdallah Ulega (Kilwa), Joshua Mirumbe (Bunda), Deodatus Kinawiro (Chunya), Rosemary Senyamule (Ileje) na Galamhusein Shaban (Mbarali).

Wengine waliobaki ni Christopher Mgala (Newala), Barika Konisaga (Nyamagana), Sara Dumba (Njombe), Hanifa Karamagi (Gairo), Halima Kihemba (Kibaha), Nurdin Babu (Rufiji), Methew Sedoyeka (Sumbawanga), Idd Kimanta (Nkasi), Chande Nalicho (Tunduru)), Senyi Ngaga (Mbinga), Wilson Nkambaku (Kishapu) na Benson Mpesya (Kahama).

Wengine ni Paul Mzindakaya (Busega), Georgina Bundala (Itilima), Fatma Toufiq (Manyoni), Luten Edward Ole Lengai (Mkalama), Hanifa Selengu (Sikonge), Seleman Kumchaya (Tabora), Mboni Mgaza (Mkinga na Seleman Liwowa (Kilindi).

Kwa  mujibu wa Pinda  wakuu wa wilaya waliofariki ni  Kapteni James Yamungu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Serengeti,Anna Magoha aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Urambo na Moshi Chang'a aliyekuwa mkuu  wa wilaya ya Kalambo. 

Wakuu wa wilaya watano waliopandishwa vyeo kuwa wakuu wa mikoa ni John Mongela aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Arusha amekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera,Amina Masenza aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Ilemela amekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa,Dk.Ibrahim Khamis aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Moshi amekuwa mkuu wa mkoa wa Katavi ,Halima  Dendego aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Tanga amekuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara na Daud Ntibenda aliyekuwa mkuu wa wilaya amekuwa mkuu wa mkoa wa Arusha.  

Waziri Mkuu Pinda amewataka wakuu wa wilaya waliobadilishwa vituo kuanza kazi mara moja huku ambapo wakuu wa wilaya ambao wanaanza kazi hiyo kwa mara kwa kwanza wakisubiri kupatiwa mafunzo ili kuboresha uwajibikaji wao.



Post a Comment