Nineneje nijivune,uneni naye Makene,
Mtambaji wa karine,bloguni jivunia.
Makene ni mtambaji, bloguni jivunia,
Chakuvunia kipaji, fasihi ziso udhia.
Japo ningile kwa kasi, bali njia kupitia,
Ili nipate wepesi,bloguni tangazia.
Kubwa lilohitajia, kiswahili kukuzia,
Ulumbi si njema njia,fasihi kutangazia.
Mikono naashiria, kuiacha hii njia,
Hima chini kuketia, nudhumu kuitumia.
Nunu sineni Makene,kwa njia ya mapene,
Kwa lako hili sebene,wastahili jivune.
Wakatabahu uneni,sitarazii mengine,
Swahili tutumieni,kufunda waso uneni.
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Nimesikia Mkwinda, nafunga wangu ugani
ReplyDeleteNimekuona kiwanda, kwa ghafi ulotunzani
Najua waweza shinda, malenga kubakiani
Mkwinda nafunga hoja, U mzima utembee.
Majibizano ya gani, utamu yanaletani
Hugeuka mtihani, malenga vina pangani
Kisha hamu hujengani, mengi shairi tungani
Mkwinda nafunga hoja, je kura umepigani?
Mimi malenga wa bara, hilo basi tambuani
Jina langu Nakuzerwa, shairini tambiani
La kaka nilichukuwa, tangu alipopishani
Diwani nikatungani, zasubiri chapishwani.
Aliitwa Benjamin, Mwalimu asoudhia
Hakutimu kipindini, Kansa ikambebani
Mkwinda ninakwambiani, imani nimejengani
Nafasi wachukuani, kaka mpya malengani!
Kaka sasa fungulia, ulotimia ugani
Utunge kuhaditrhia, ujio wao wageni
Lugha wanachafulia, dhahabu sumu wekani
Nakimbia darasani, mtihani kufanyia.
Nimesikia Mkwinda, nafunga wangu ugani
ReplyDeleteNimekuona kiwanda, kwa ghafi ulotunzani
Najua waweza shinda, malenga kubakiani
Mkwinda nafunga hoja, U mzima utembee.
Majibizano ya gani, utamu yanaletani
Hugeuka mtihani, malenga vina pangani
Kisha hamu hujengani, mengi shairi tungani
Mkwinda nafunga hoja, je kura umepigani?
Mimi malenga wa bara, hilo basi tambuani
Jina langu Nakuzerwa, shairini tambiani
La kaka nilichukuwa, tangu alipopishani
Diwani nikatungani, zasubiri chapishwani.
Aliitwa Benjamin, Mwalimu alosheheni
Hakutimu kipindini, Kansa ikambebani
Mkwinda ninakwambiani, imani nimejengani
Nafasi wachukuani, kaka mpya malengani!
Kaka sasa fungulia, ulotimia ugani
Utunge kuhaditrhia, ujio wao wageni
Lugha wanachafulia, dhahabu sumu wekani
Nakimbia darasani, mtihani kufanyia.
karibu ndugu MKWINDA
ReplyDeletetuso kauli
ReplyDeletewala ilihali
mizani imegoma akilini.
Yetuye macho!