Ads (728x90)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitangaza baraza lake la mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam jana Desemba 10, 2015. Kulia kwake ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na kushoto ni Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa.
Jana Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Magufuli anatangaza baraza la mawaziri wa Jamhuri wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Tuwe pamoja kulifahamu baraza letu.
Magufuli: Kumekuwa na speculation nyingi na watanzania wamekuwa na hamu kubwa ya kujua baraza la mawaziri, baada ya kusubiri kwa muda mrefu, baada ya kuapa tulitakiwa angalau tarehe kumi tuwe tumetangaza baraza.
Tuliona angalau tujiridhishe kwanza, baraza lililopita lilikuwa na mawaziri na manaibu zaidi ya 59, tukaona tuwe na baraza dogo. Hatuwezi kukaa bila baraza, katika baraza hili, wizara nyingi tumeziunganisha na kutakuwa na wizara 18 na tutakuwa na mawaziri 19 tu, kuna baadhi ya wizara zitakuwa na mawaziri na hazitakuwa na manaibu waziri.
Lengo ni kutimiza ahadi yetu ya kuwa na baraza dogo kupunguza gharama na effective kwa kufanya kazi. Zilitengwa bilioni 2, mawaziri watakapoteuliwa waende semina elezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure. Watafanya semina elekezi wenyewe ndani kwa ndani.
BARAZA LA MAWAZIRI
WIZARA OFISI YA RAIS,TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA.
Mawaziri - George Simbachawene  na Angella Kairuki
Naibu Waziri - Sumeilam Jafo. Naibu.
WIZARA  OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA
Waziri - January Makamba
Naibu Waziri – Luhaga Jerrson Mpina



OFISI YA WAZIRI MKUU SERA,BUNGE,KAZI VIJANA, AJIRA NA WALEMAVU
Waziri - Jenista Muhagama
MaNaibu – Dkt. Possy Abdallah na Anthony Mavunde.
WIZATA KILIMO MIFUGO NA UVUVI
Waziri - Mwigulu Nchemba
Naibu Waziri - William Ole Nasha
WIZARA YA UJENZI,UCHUKUZI NA MAWASILIANO
(waziri Bado hajapatikana).
Naibu Waziri – Inj. Edwin Amandusi Ngonyani



WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
(Waziri Bado hajapatikana).
Naibu Waziri - Ashantu Kizachi


WAZIRI WA NISHATI NA MADINI

Waziri - Prof. Mwijarubi Muhongo.
Naibu Waziri - Medalled Karemaligo.



WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
Waziri - Harrison Mwakyembe
WAZIRI WA MAMBO YA NJE, USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI,KIKANDA NA KIMATAIFA.
Waziri - Dk. Augustino Mahiga
Naibu Waziri – Dkt. Susan Kolimba.



WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
Waziri - Dk. Hussein Mwinyi


WIZARA YA MAMBO YA NDANI
Waziri - Charles Kitwanga.



WIZARA YA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI.
Waziri - William Lukuvi
Naibu Waziri - Angelina Mabula



WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
(Waziri Bado hajapatikana).
Naibu Waziri– Inj. Ramol Makani



WIZARA YA VIWANDA,BIASHARA NA UWEKEZAJI.
Waziri Charles Mwijage.



WIZARA YA ELIMU,SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI
(Waziri Bado hajapatikana).
Naibu Waziri – Inj. Stella Manyanya
WIZARA YA AFYA MAENDELEO YA JAMII,JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Waziri - Ummy Mwalimu
Naibu Waziri –  Dkt. Hamis Kigwangala



WIZARA YA HABARI,UTAMADUNI,WASANII NA MICHEZO
Waziri - Nape Nnauye
Naibu Waziri - Anastasia Wambura.
WIZARA YA MAJI NA UMWAGILIAJI
Waziri – Prof. Makame Mbarawa
Naibu  Waziri– Inj. Isack Kamwela

( KWA HISANI YA MTANDAO JOSEPHAT LUKAZA BLOG)

Post a Comment