Ukitumika vyema, itaongoka jamii,
Ikiwa bora kusema,yako huyazingatii,
Insi watajalalama,Kwa kuikosa shafii,
Mdomo wata kunena,yaso yako kunenea.
Kinenea neno jema, wanenewao tatii,
Watakwenzi maulama', walopata digirii,
Uta'wa mja wa wema, uloshinda makarii,
Mdomo wata kunena, yaso yako kunenea.
Nenolo litatuama,makarii watatwalii,
Litaja dumu dawama, japo utakuwa zii,
Umeacha chumo jema, kaburi hulijutii,
Mdomo wata kunena, yaso yako kunenea.
Nena neno lenye dhima,lijesomwa kwa bidii,
Walinene watu wema, watawao ja sufii,
Lije kuongowa umma,urithi wa manabii,
Mdomo wata kunena,yaso yako kunenea.
Enyi mpendao sema chungeni kauli hii,
Midomo yenu gharama,iwapo hufikirii,
Msijepata lawama,ikiwa hamchungii,
Mdomo wata kunena,yaso yako kunenea.
Mdomo nacha kusema, kauli siifichii,
Hapa bora kutuama,niwacheni wenye fii,
Bali waadhi ni mwema,ijapo hamtulii,
Mdomo wata kunena,yaso yako kunenea.
Wakatabahu.
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment