TA, TE, TI, TO, TU.
TA:Nataataa na tata,watatue watatuzi,
Sitati kimtang'ata, kwa tata za utatizi,
Nitatapo Kimvita,watatwao watatezi,
Mahiri wa utatizi, tutete na tungo TATA.
TE: Niteetapo na tete, siteti penye terezi,
Hateta hadi utete, nitete na watetezi,
Nije teta kiutete, nimetemete ja mwezi,
Mahiri wa utatizi, tutete na tungo TATA.
TI:Ja burudi ya tikiti, tungo njema ndizo hizi,
Lahamu yake ya kati,ni tamu kushinda ndizi,
Ulilapo katikati, watarazia uchizi,
Mahiri wa utatizi,tutete na tungo TATA.
TO:Natongoa mitopoto, ilotopea kwa kwa wazi,
Kauli za kilipyoto,zatotesha fasihi enzi,
Beti tele za upoto, kurasa zinabarizi,
Mahiri wa utatizi, tutete na tungo TATA.
TU:Tamati Ta, Te, Ti,To, Tu,tungo TATA sendelezi,
Sijateta kwa mtutu, bali tati za ujuzi,
Kuwafunda watukutu, fasihi wasomaizi,
Mahiri wa utatizi, tutete na tungo TATA.
Wakatabahu
Recent Posts
- Rashid Mkwinda03 Sep 2017NaViNjArI TaNzANiA- NILIPOTEMBELEA RAFIKI ZANGU WA KIMAASAI
Nipo na rafiki zangu jamii yaWamaasai tukibadilishana mawazo Nimetembelea rafiki zan...
- Rashid Mkwinda16 Aug 2017SOKO LA SIDO JIJINI MBEYA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA USIKU
Eneo la Soko la SIDO jijini Mbeya lilivyokuwa likiteketea kwa moto jana usiku Sok...
- Rashid Mkwinda19 Jul 2017MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA MKE WA DKT MWAKYEMBE KYELA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mke wa Dkt Ha...
- Rashid Mkwinda18 Jul 2017MWILI WA MRS MWAKYEMBE WAWASILI MBEYA JIONI HII, MSAFARA KUELEKEA KYELA
Viongozi wa serikali wa mikoa ya Mbeya na Songwe mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mk...
- Rashid Mkwinda16 Jul 2017RAIS DKT MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KIFO CHA MKE WA DKT. MWAKYEMBE
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...
- Rashid Mkwinda30 Jan 2017GOLIKIPA DAVID BURHANI AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa Golikipa wa kutegemewa wa timu za Majimaji ya Songea,Prison na Mbeya Ci...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mkwinda: umekuja na mpya kabisa. Ta, te, ti, to, tu. Sawa malenga wetu. Usiwe unapotea namna hii.
ReplyDeleteNDA: Nda kauliyo Mkwinda hinitiya mato giza
ReplyDeleteNDE: Mamvitani chonde chonde, nti huno hutereza,
NDI:Fasihi haina mshindi, na wamrima waiweza,
NDO: Hisikiyapo ndo ndo ndo, nsondo huno sitateza
NDU: Watukutu si watundu, ntundu hucha kujikweza
Nda! nde! ndi! ndo! ndu! mdundo, Ubeti watosheleza,
Ndiye nzuri wa nyendo, kurasa nacha kujaza
asante Mwandani,kwa fikrezo makini,
ReplyDeletempashe mkwindani,amekuwa mwanajini,
mara ta mara ten,kama yuko mautini,
anatatarika nini,ka sio malengani!
kwa nini anajihini,kutunganiblogun
ndesanjo yu mashakan,kuingia hatiani,
ni sawa na kumkundi,nje mwa kasrini
anatatarika nini, ka sio malengani!
wa zenjin mrimani,hata kule mombasani,
kote tumo utatani,kwa hii tata tatani,
nashindwa pata baini,nini hasa atungani,
anatatarika nini,ka sio malengani!
sasa makene baini,umtoe tatarani,
kijana wako shetani,aso haya wala soni,
si mwingine rashidani,aondoka ulengani
anatatarika nini,ka sio malengani
naondoka postini,ni mgeni fasihini,
sije anza chokoani,bata akanishindani
Mkwinda sasa adhini,nami tayari swalani,
anatatarika nini,ka si malengani
mh!
ReplyDeletekazi kwelikweli,hii fani itabidi niulize chuo chake maana yataka moyo,ta te ti to tu,nda nde ndi ndo ndu,
inawezekana wameanza kutafuta maana ya blog kwa njia ushairi hawa tuendelee tuone!
mzee pink noma. chagua color ya kiume.
ReplyDeleteNimekuona Nyembo, kwa zako nyimbo,
ReplyDeleteLakini ndio mwendo,bali acha majigambo,Ukiingia katika fani, utanata kama urimbo,usijifutue ja Tembo, ukaharibu huu mtambo.
Huu ni ghali mtambo,
Asiliye ni ng'ambo,
Hivyo chukua tahadhari Nyembo.
Tulia nakujia na kitu kingine nadhani ni kweli tuko katika safari ya kulisaka neno mbadala kwa hili la Blogu tulia sikia vyombo tazama katika blogu kuna CHACHANDU ZA UCHACHIZI.