Ads (728x90)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA
Kumb. Na EA.7/96/01/B/130 25 Mei, 2012
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki, pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi ya Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 2285 za kazi kwa waajiri mbalimbali kama ifuatavyo:
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sanyansi na Teknolojia, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Msajili Mahakama ya Rufaa, Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Lindi, Manyara, Kigoma, Arusha, Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Tabora, Morogoro na Rukwa.
Katibu Tume ya Utumishi wa Umma, Katibu, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Katibu Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Katibu Tume ya Pamoja ya Fedha, Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Msajili wa Vyama vya Siasa, Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA), Mtendaji Mkuu Wakala wa Barabara Tanzania, Mtendaji Mkuu Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania, Mtendaji Mkuu Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. 2

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Mwanza. Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Mtwara, Singida, Sumbawanga, Morogoro, Songea, Kigoma/Ujiji na Temeke. Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Bunda, Chato, Chamwino, Handeni, Songea, Bahi, Kibaha, Pangani, Tunduru, Mkuranga, Mafia, Mufindi, Njombe, Mwanga, Nachingwea, Nkasi, Masasi, Monduli, Mtwara, Ruangwa, Rufiji, Bukoba, Tandahimba, Same, Tarime, Kibondo, Biharamulo, Newala, Simanjiro, Kondoa, Ngara, Mpanda na Halmashauri ya Mji wa Njombe.
NB: Aidha, tangazo hili linapatikana kwenye tovuti zifuatazo: www.ajira.go.tz, www.utumishi.go.tz na www.pmoralg.go.tz
1.0 AFISA UTUMISHI DARAJA LA II (HUMAN RESOURCES OFFICER GRADE II) – NAFASI 30

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Katibu Tume ya Utumishi wa Umma, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Rukwa. Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara na Singida, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Rufiji, Handeni, Mkinga, Ngara, Songea, Bahi, Newala na Halmashauri ya Jiji la Mwanza
1.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kutunza Kumbukumbu sahihi za watumishi wote katika Wizara, Mikoa, Wilaya na Idara zinazojitegemea kulingana na mahali alipo.
 Kutafsiri na kushughulikia utekelezaji wa miundo ya utumishi.
 Kutafiti, kuchanganua na kukadiria idadi ya watumishi wanaohitaji mafunzo.
 Kuandaa na kupanga mipango ya mafunzo ya muda mfupi na mrefu.
 Kukadiria na kupanga mahitaji ya vifaa vya mafunzo kwa kushirikiana na vyuo vilivyopo chini ya sekta zinazohusika.
 Kukusanya, kuchambua na kupanga takwimu na kumbukumbu zote zinazohusu mipango ya watumishi.

1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza ya Sayansi Jamii au Sanaa kutoka katika Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali ambao wamejiimarisha (major) katika mojawapo ya fani zifuatazo:-
§ Menejimenti ya Raslimali Watu (Human Resources Management).
§ Elimu ya Jamii (Sociologly).
§ Utawala na Uongozi (Public Administration).
§ Mipango ya Watumishi (Manpower Planning).
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
3


1.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
2.0 AFISA TAWALA DARAJA LA II (ADMINISTRATIVE OFFICER GRADE II) – NAFASI 14

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Pwani, Lindi, Mtwara, Manyara, Rukwa na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.
2.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kusajili vizazi, vifo na ndoa na kutoa hati za viapo.
 Kuweka kumbukumbu za matukio muhimu,
 Kuwapokea na kuwahoji wakimbizi wanaowasili,
 Kuweka kumbukumbu za Wakimbizi
 Kutunza na kugawa vifaa vya wakimbizi katika makazi.
 Kuainisha, kuchambua na kushauri kuhusu matatizo ya wakimbizi.
 Kusimamia nidhamu ya wakimbizi.
 Kusimamia utekelezaji wa Sheria, Sera, Kanuni na Taratibu mbalimbali Serikalini kutegemeana mahali alipo.
 Kusimamia kazi za utawala na uendeshaji katika ofisi za Serikali.
 Kutoa vitambulisho kwa wakimbizi.
2.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika fani zifuatazo:- Utawala, Elimu ya jamii, Sheria (baada ya internship), Menejimenti ya Umma
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
2.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
3.0 AFISA KUMBUKUMBU DARAJA LA II (RECORDS OFFICER GRADE II) – NAFASI 2

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.
3.1 MAJUKUMU YA KAZI

Hili ni daraja la mafunzo katika kazi hivyo atafanya kazi kwa maelekezo ya Maafisa Kumbukumbu walio juu yake kwa cheo. Kazi atakazojifunza na kufanya ni zile zifanywazo na Afisa Kumbukumbu Daraja la I:-
 Kudhibiti mifumo ya kumbukumbu, kutunza, na kusimamia matumizi ya kumbukumbu.
 Kutambua na kutafuta kumbukumbu katika masjala.
4


Kudhibiti mfumo wa kumbukumbu zinazozalishwa na kompyuta, kutunza na kusimamia matumizi yake.

3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa mwenye Shahada ya Kwanza katika fani ya Utunzaji na Uhifadhi wa Kumbukumbu (Records management & Archieves), Upimaji na Ramani na nyingine zinazolingana nayo kutoka katika Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali. Aidha wawe na ujuzi wa kutumia kompyuta.

3.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali TGS D kwa mwezi.
4.0 MTAKWIMU DARAJA LA II (STATISTICIAN GRADE II) – NAFASI 14

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Rukwa, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Tunduru, Rufiji, Mkuranga na Newala.
4.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kubuni na kuendeleza mfumo wa kitaifa wa kukusanya na kuratibu takwimu
 Kutengeneza utaratibu wa kukusanya takwimu pamoja na ule wa kuchukua takwimu za mfano/vielelezo (Sampling)
 Kukusanya, Kuchambua na kuwasilisha takwimu ngazi za juu.

4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza katika fani ya Takwimu au Hisabati au sifa zinazolingana na hizo kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia “Information Communication Technology (ICT)

4.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
5.0 MTAKWIMU MSAIDIZI (ASSISTANT STATISTICIAN ) – NAFASI 1

Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi
5.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kukusanya Takwimu ( Data)
 Kuchambua na kukagua fomu za maswali zilizokwishajazwa na kujibiwa.

5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye cheti (Certificate) cha Takwimu kutoka Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki (The Eastern Afrika Statistical Training Center) au vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali wenye ujuzi wa kutumia kompyuta (ICT)
5


5.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
6.0 KATIBU WA KAMATI DARAJA LA II (COMMITTEE CLERK GRADE II) – NAFASI 13

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, Mkinga, Tunduru, Mwanga, Newala, Mkuranga na Nkasi.
6.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandaa ratiba ya vikao vyote vya Halmashauri na kamati zote kwa kushauriana na Mkurugenzi Mtendaji
 Kuandika Mihutasari ya vikao vya Halmashauri
 Kuweka Kumbukumbu za vikao vya Halmashauri nma kamati zake.
 Kutunza Vifaa vyote vinavyohusiana na mikutano.
 Kuhifadhi orordha ya mahudhurio ya Madiwani na Wataalamu.
 Kutoa ratiba ya ufuatiliaji na utekelezaji wa maazimio
 Kutunza Kanuni za Mikutano.
 Kusimamia “cutting” za mihutasari.

6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada /Stashahada ya Juu ya Sheria/Sanaa/ Utawala kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

6.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D kwa mwezi.
7.0 AFISA MIPANGO MIJI DARAJA LA II (TOWN PLANNER) – NAFASI 17

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Tabora, Rukwa, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mtwara, Singida, Sumbawanga, Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Handeni, Nachingwea, Rufiji, Mafia, Morogoro, Pangani na Tunduru.
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandaa mipango ya maeneo yaliyoendelezwa kiholela.
 Kuandaa michoro ya Mipangomiji.
 Kupokea michoro ya Mipangomiji na taarifa za maeneo ya ardhi yanayopendekezwa kuiva kwa ajili ya uendelezaji kimji.
 Kuchambua takwimu na taarifa kwa ajili ya maandalizi ya mipango mipya ya makazi.
 Kupokea na kuweka kumbukumbu za maombi ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi na umegaji wa viwanja.
 Kuhakikisha kuwa mabadiliko ya matumizi ya ardhi yanaingizwa katika michoro.

7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
6

Kuajiriwa mwenye Stashahada ya juu/Shahada katika fani ya Mipangomiji kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi au Vyuo Vikuu au Taasisi nyingine zinazotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.
8.0 MSAIDIZI WA MTENDAJI MKUU DARAJA LA II (EXECUTIVE ASSISTANT GRADE II) – NAFASI 1

Nafasi hii ni kwa ajili ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu
8.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na siri
 Kupokea wageni na kuwasaili shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
 Kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi na kumuarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitajika.
 Kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachoitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.
 Kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.
 Kuyapokea majalada, kuyagawa kwa maofisa walio katika sehemu alipo, na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusikika.
 Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya vikao mbalimbali mahali alipo.
 Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi na kuifikisha sehemu zinazohusika na upatikanaji wa vifaa hivyo.
 Kuwapangia na kuwaelekeza kazi Makatibu Mahsusi walio chini yake.
 Kuwasaidia Makatibu Mahsusi walio chini yake kuhusu matumizi ya mashine za kazi na utunzaji wake.
 Kutoa na kufuatilia panapohusika kuhusu matengenezo ya mashine za kazi.
 Kuandika muhutasari wa vikao vinavyohusika sehemu alipo na kufuatilia utekelezaji wa maamuzi ya vikao hivyo.
 Kuandika barua zinazotoa taarifa ya ratiba ya shughuli au safari za Mkuu wake na kuitisha vikao.
 Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wake sehemu mbalimbali

8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa mwenye Stashahada ya kawaida ya Uhazili itolewayo na Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) au chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali ambaye amehudhuria mafunzo ya kompyuta na kupata cheti katika programme za Window, Microstoft Office, Internet, E-mail na Publisher. Pia, Awe na uzoefu wa kazi kwa muda usiopungua miaka kumi na mbili. Aidha, Awe Amehudhuria na kufaulu mafunzo
7


ya Menejimenti kwa ajili ya Wasaidizi wa Watendaji Wakuu kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) au vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

8.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS F kwa mwezi.
9.0 AFISA USIMAMIZI WA FEDHA DARAJA LA II (FINANCE MANAGEMENT OFFICER II) - NAFASI 2

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Tawala Mkoa wa Tanga na Mtwara
9.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandikisha na kudhibiti Amana (Securities) za Serikali.
 Kufuatilia hati za hisa.
 Kuwasiliana na watoaji mikopo/misaada kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa miradi.
 Kuweka kumbukumbu za madeni ya nje.
 Kuweka kumbukumbu za mikopo ya ndani.
 Kufuatilia na kusimamia matayarisho ya makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali.
 Kufuatilia utayarishaji na uchambuzi wa “Flash Reports” za kila mwezi.

9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya Sanaa yenye mwelekeo mkubwa katika fani ya Uchumi na Mipango (Major in Economics) au Biashara au Sheria (LL.B) au Stashahada ya Juu ya Uhasibu au Uchumi & Mipango au Biashara au Stashahada ya juu ya Usimamizi wa kodi kutoka Chuo/Taasisi inayotambuliwa na Serikali.
 Waombaji wenye Cheti cha Taaluma ya Uhasibu CPA (T) au sifa nyingine inayolingana na hiyo inayotambuliwa na NBAA watafikiriwa kwanza.

9.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.D kwa mwezi
10.0 MHAKIKIMALI DARAJA LA II (STOCK VERIFIER GRADE II) - NAFASI 5

Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha
10.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kukagua bohari za kati za Serikali na kutoa taarifa za ukaguzi.
 Kutathmini na Kuchambua hoja muhimu zilizomo katika taarifa za uhakikimali.
 Kufanya uchambuzi wa taarifa za ‘Boards of Survey’ na kutoa mapendekezo juu ya utekelezaji wake.
 Kutunza daftari la taarifa za upotevu, ajali, fidia, vitunzia fedha (cash receptables), usajili wa magari ya Serikali na uahalisho (respective approval).

10.2 SIFA ZA MWOMBAJI

Post a Comment

  1. หนังแอคชั่น หนังใหม่ ดูหนังฟรีต้อง Alita: Battle Angel อลิตา แบทเทิล แองเจิ้ล (2019) สนุกกว่าใครที่เว็บดูหนังเว็บนี้

    https://www.doonung1234.com/

    ReplyDelete