Ads (728x90)

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Kanali Chiku Gallawa wakiangalia Kupatwa kwa Jua eneo la Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya leo asubuhi Jua limepatwa leo kuanzia saa 4:15 hadi saa 7:00 mchana.
Mkazi wa Rujewa akiangalia kupatwa kwa jua kwa kutumia mashine ya kuchomolewa vyuma'Welding' wakati wa kupatwa kwa jua leo mchana.


Raia wa kigeni kutoka nchi za Ujerumani, Uingereza na Sweden wakitumia chombo maalumu cha kuchuja mionzi ya Jua kwa ajili ya kuangalia kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Hivi ndivyo kupatwa kwa jua kulivyokuwa kukionekana kwa kupitia chujio maalum la kuchuja mionzi ya jua.

Mkazi wa mjini Rujewa akiangalia kupatwa kwa jua kupitia miwani ya kuchujia mionzi ya jua leo asubuhi.

Mkuu wa wilaya ya Mbarali Reuben Mfune akizungumza wakati wa kupatwa kwa jua mjini Rujewa wilayani Mbarali.

Mbunge wa Mbarali Haroun Pirmohamed akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) Christopher Nyenyembe

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari wakishuhudia kupatwa kwa jua leo asubuhi

Post a Comment