| Njiani tulishuhudia namna ambavyo Mwenyezi Mungu alivyoumba dunia kwa kuweka milima iliyofanana na vigingi vilivyosimikwa ardhini kuisimamisha dunia. |
| Tulisafiri kwa mwenda mrefu tukasimama kuchimba dawa katika baadhi ya nyumba katika kijiji kimoja cha Luwawa wilayani Mzimba mkoa wa Kaskazini. |
| Baadhi ya nyumba za maeneo haya kijiji cha Luwawa WILAYA ya Mzimba nchini Malawi ni sawa na baadhi ya nyumba za vijiji vya TANZANIA |
| Tulivutiwa na uchomaaji wa mbuzi kwa njia ya kukaanga kwenye karai tulitafuna nyama ya mbuzi kutuliza njaa |
| Tulifika katika mji maarufu wa Jenda hapo tulipata fursa ya kupumzika kidogo, ni safari ya kuelekea Jijini Lilongwe, ilikuwa ni safari nzuri ya kuvutia. |
Post a Comment