Ads (728x90)


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Mkalla akiwa na viongozi wa kitaifa wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) mara baada ya kikao chake na baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya leo mchana


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanahabari wa mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa leo mchana
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akiwa na Katibu Tawala wa Mkoa Mariam Mtunguja alipokutana na wanahabari wa mkoa wa Mbeya leo mchana
Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano wa TAJATI Felix Mwakyembe akizungumza jambo mbele ya mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla kwenye ukumbi wa Mkapa leo mchana
 
Mwenyekiti wa Kitaifa wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) Ulimboka Mwakilili akisisitiza jambo wakati wa kikao kilichomhusisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla na baadhi ya wanahabari wa mkoa wa Mbeya

Makamu Mwenyekiti wa TAJATI Christopher Nyenyembe akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla kwenye ukumbi wa Mkapa leo mchana
-Awataka waandike habari za kweli zenye changamoto
-Asisitiza hakuja Mbeya kufanya siasa
MKUU wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla ametoa somo kwa wanahabari akiwataka waibue habari za kweli na zenye changamoto zitakazoisadia serikali huku akijitanabahisha mbele yao kwamba amekuja mkoani Mbeya kwa ajili ya kufanya kazi na wala hakuja kufanya siasa.
‘’Nataka wanasiasa wajue kuwa mie sifanyi siasa bali nimekuja kufanya kazi, najua wazi kuwa Jiji la Mbeya na halmashauri yake iko chini ya upinzani,wanasiasa wafanye siasa zao mie ninafanya kazi,’’alisema
Alibainisha kuwa kamwe hatahusisha utendaji wake na mambo ya siasa ingawa baadhi ya wanasiasa wanadhani utendaji wake unashinikizwa na kasi za kisiasa,’’alifafanua.
‘’Mie ni mtoto niliyekulia Baracks Police, baba yangu na mama yangu walikuwa ni askari polisi, wote wameshatangulia mbele ya haki, Baba yangu aliniusia Nikipewa nifanye kikweli kweli, na kiukweli ninapopewa kazi nafanya kazi kila nilipopewa majukumu huwa natimiza wajibu wangu i am serious nimekuja kufanya kazi sio siasa,’’alisisitiza.
Sanjari na azma yake hiyo ya kufanya kazi pia amewataka wanahabari kushiriki katika kuibua changamoto zilizopo ili ziweze kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Mbeya katika nyanja za kiuchumi na kijamii.
Akizungumza katika kikao maalum na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Mkapa, Makalla alisema wanahabari ni sekta muhimu inayoweza kuisaidia serikali katika kuibua mambo ya msingi ambayo yanaweza kuchukuliwa na kufanyiwa kazi na serikali.
‘’Tusaidiane mnapoona mapungufu serikalini, andikeni hata habari zenye changamoto bali andikeni habari zenye ukweli,’’alisema Makalla.
Aidha Makalla ameelezea changamoto mbalimbali za utendaji zilizopo kwa watumishi wa umma huku akiweka bayana tatizo la watumishi hewa ambalo limeisababishia hasara serikali na kuwa amedhamiria kurejesha dhana ya utumishi bora kwa watumishi wa umma.
Awali Mkuu huyo wa Mkoa alipokea taarifa mbalimbali zenye changamoto kutoka kwa waandishi wa habari kutokana na utendaji baina ya wanahabari na ofisi ya mkuu wa mkoa ikiwa ni pamoja matatizo ya watendaji wa halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ugawaji viwanja holela katika maeneo ya wazi.

Post a Comment