Ads (728x90)



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Christopher Kilungu
Minazi zao ambalo Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo inataka kulifanya kuwa ni zao la biashara
Mbali na minazi yapo mazao mengine ambayo yakiimarishwa na kuzalishwa kwa wingi yanaweza kuwa ni chanzo cha mapato wilaya ya Namtumbo kama vile zao la Embe za mbegu za miti mifupi na mbegu za miti mirefu



HALMASHAURI ya wilaya ya Namtumbo imetenga bajeti ya Sh milioni 10  kwa msimu wa kilimo wa 2016-17 ili kuimarisha zao la Korosho na minazi liweze kuongeza tija kwa wakulima na kipato kwa Halmashauri ya wilaya hiyo.

Mazao ya Minazi na Korosho ambayo yamezoeleka kulimwa katika mikoa ya Pwani yanatarajiwa kuongeza pato la Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo baada ya kuonekana uwezekano mkubwa wa kustawi katika maeneo ya Kata za Magazini,Lusewa,Likuyuseka na Kijiji cha Mandepwende.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Christopher Kilungu alisema kuwa mkakati huo ni kwa ajili ya kuongeza uwekezaji katika mazao ya biashara yenye uwezekano mkubwa wa kustawi wilayani humo.

Alisema Halmashauri katika bajeti yake ya mwaka 2016/17 imetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa mbegu na miche bora ya mazao ya biashara ili kuwagawia wakulima kwa nia ya kuongeza uzalishaji wa mazao hayo na hatimaye kuongeza kipato cha mkulima mmoja mmoja na kwa Halmashauri.

Kitundu alisema jumla ya miche 5000 ya minazi ambayo itanunuliwa mkoani Mtwara itaanza kugaiwa kwa wakulima waanze kuzalisha zao hilo ili kuepuka kufuata nazi katika mikoa ya Pwani jambo ambalo limekuwa ni gharama kubwa kwa wafanyabiashara na kulifanya zao hilo kuuzwa kwa bei ya juu.

‘’Kwa utafiti wetu zao hili linastawi zaidi katika ukanda wa kusini maeneo ya Mchomoro,Rwinga, Lusewa,Magazini, Likuyu na Msisima,tumepanga kutumia shilingi  milioni 5 kwa ajili kununua miche kutoka Mtwaram’’alisema Kitundu.

Sanjari na zao la Minazi Kitundu alisema Halmashauri pia imepanga kutumia sh. Milioni 5 kwa ajili ya kununua miche ya zao la Korosho ambalo limeonekana kuwa na tija kwa wakulima kwa kipindi hiki.

Mazao mengi ya biashara ambayo alisema yanaweza kuibua uwekezaji katika sekta ya kilimo ni pamoja na Kahawa,Soya,Tangawizi,Mpunga,Choroko, Mbaazi na Ufuta ambapo baadhi ya mazao kama vile Soya limeshapata mnunuzi kampuni ya Silverland ya mkoa wa Iringa ambaye ameahidi kununua tani 9,000 hadi 11,000 kwa bei ya sh.1,000 badala ya sh.750 iliyokuwa ikiuzwa msimu uliopita.


Post a Comment