Ads (728x90)


Mmoja wa washitakiwa akiwa ameanguka chini mahakamani kabla ya kuahirishwa kesi kwa mara ya kwanza, kesi inayowahusu imamu na mganga wa kienyeji wakishtakiwa kwa uchomaji wa Koran Tukufu


Baadhi ya waumini wa Kiislamu wakiwa wamekusanyika katika mahakama ya wilaya Namtumbo kusikiliza kesi kabla haijaahirishwa wiki iliyopita, kesi hiyo itaanza kusikilizwa kesho Disemba Mosi


Waumini wa Kiislamu wakisoma dua kumuomba Mwenyezi Mungu kufuatia kitendo cha Uchomaji Koran kilichodaiwa kufanywa na watu kwa aimani ya ushirikina

Na Mwandishi Wetu, Namtumbo
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma kesho inatarajia kuanza kusikiliza kesi inayowakabili waumini sita wa dini hiyo wanaokabiliwa na kesi ya uchomaji wa Kor an Tukufu baada ya kuahirishwa siku 10 zilizopita kwa madai kuwa  mshitakiwa namba mbili Shazir Rashid (31) kuelezwa mahakamani hapo kuwa ameugua ghafla ugonjwa wa kifafa.

Kesi hiyo ya jinai namba 48 iliahirishwa mara ya kwanza Novemba 11, 2016, baada ya mshitakiwa namba moja Rashid Ausi(75) kuanguka kizimbani kwa kile kilichoelezwa kuwa mshitakiwa huyo aliugua ghafla maradhi ya tumbo.

Madai ya mshitakiwa wa pili wa kesi hiyo kukumbwa na ugonjwa wa kifafa  ilimsababisha Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Majinge Kusaga kuahirisha tena kesi  hiyo hadi jana ambapo pia imeahirishwa tena hadi Disemba Mosi baada ya mshitakiwa mwingine kushindwa kufika mahakamani kwa madai ya kuugua ugonjwa wa kifafa.

Mara baada ya washitakiwa wote sita kuitwa mahakamani kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo orodha ya washitakiwa haikutimia badala ya washitakiwa sita waliopaswa kupanda kizimbani walionekana washitakiwa watano ndipo hakimu Majinge alitaka kujua alipo mshitakiwa namba mbili wa kesi hiyo.

Hakimu Majinge alimuita mdhamini wa mshitakiwa huyo Cladius Fungo ambaye aliithibitishia mahakama hiyo kuwa mshitakiwa namba mbili Shazir Rashid anaumwa ameanguka ugonjwa wa kifafa huko kijijini.
Baada ya maelezo hayo Hakimu Majinge alilazimika kuahirisha kesi hiyo hadi Disemba Mosi ambapo kesi hiyo italetwa tena mahakamani kwa ajili ya kuanza kutolewa ushahidi.

Katika hatua nyingine kundi kubwa la waumini wa dini ya Kiislamu ambao walihudhuria mahakamani hapo waliendelea kusimama wakionesha dalili za kupata maelezo zaidi ya kuahirishwa kwa kesi hiyom ndipo mmoja wa maaskari alitoa ufafanuzi na kuwaeleza waumini hao kesi hiyo imeshindwa kusikilizwa kutokana na mshitakiwa namba mbili kushindwa kufika mahakamani kwa maelezo kuwa anaumwa.

Mara baada ya waumini wa dini hiyo kuondoka mahakamani hapo walirejea katika msikiti mkuu wa wilaya ambapo kwa pamoja waliamua kufanya dua kwa kile walichoeleza kuwa wanaomba usaidizi kwa Mwenyezi Mungu juu ya tukio zima la uchomaji wa Koran lilivyofanyika.

Kaimu Shekhe wa wilaya hiyo Ahmad Banda alisema kuwa wanamtumia jukumu hilo Mwenyezi Mungu ili kuepusha laana ambayo anaweza kuishusha kuathiri watu wasio na hatia.

Shekhe Banda alisema kitendo kilichofanyika cha uchomaji Kor an kinaweza kuleta balaa kwa jamii, ili laana isiwakute wasiohusika na kwamba wameamua  kufanya dua na kuwa wataendelea kufanya dua kila Ijumaa, kumlilia Mwenyezi Mungu.

Post a Comment