Ads (728x90)


UZINDUZI wa kampeni za uchaguzi CCM kata ya Kiwira wilayani Rungwe umeingia na dosari baada ya mmoja wa mashabiki wa chama hicho Frank Mwasanu(19)aliyekuwa akiendesha pikipiki kujiingiza katika Hiace yenye namba za usajili T 527 AEP na kufa papo hapo.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 8:00 mchana wakati wa shamra shamra za kampeni za mgombea wa CCM Peter Nkanje ambapo makundi ya watu walikuokuwa ndani ya pikipiki walikuwa wakivinjari huku na huko katika harakati za kupamba uzinduzi wa kampeni hizo.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa marehemu alikuwa na kundi la wafuasi wa chama chake ambao walikuwa wakikimbiza pikipiki kwa mwendo wa kasi na baadaye kijana huyo alijiingiza chini ya mvungu wa Hiace ambayo ilikuwa ikielekea Tukuyu.......

Post a Comment