Nimeshuhudia barabara hiyo ikiwa na mahandaki kiasi cha kusababisha baadhi ya magari yanayopita njia hiyo kukwepa pembeni na kuharibu ladha yote ya safari kwa wasafirishaji na abiria waliomo katika vyombo vya usafiri wanavyotumia. |
![]() |
Kwa kuangalia haraka haraka unaweza kudhani ni maua yamechorwa katika barabara hii, La hasha haya si maua bali ubovu wa barabara iliyotengenezwa na Kampuni moja ya Kichina. |
![]() |
Awali mara baada ya kukamilika kwa barabara hii madereva na wasafiri walikuwa wakijivunia kupita katika barabara hii lakini kwa sasa imekuwa ni machungu kwa magari kukutana na adha ya mahandaki. |
![]() |
Barabara inavyoonekana baada ya kuanza kutumiwa |
![]() |
Barabara kati ya Stendi Kuu na Meta inavyoonekana pichani. |
![]() |
Gari likijitahidi kupita kwa uangalifu katika mahandaki yaliyopo katika barabara mpya iliyokabidhiwa na kuanza kutumika kama inavyoonekana pichani. |
![]() |
Viraka katika barabara ya Stendi Kuu hadi Meta inavyoonekana |
![]() |
Hivi ndivyo inavyoonekana barabara hiyo kama ilivyokutwa leo asubuhi na paparazi wetu aliyeamua kujiridhisha na kutembea hatua kwa hatua kujionea hali halisi ya barabara hiyo. |
![]() |
Viraka vya barabara mpya iliyokabidhiwa na kuanza kutumika hivi karibuni |
![]() |
Hapa ni eneo la Mabatini ambako barabara hiyo iliyogharimu fedha za walipa kodi imepita kuelekea karibu na Hospitali ya wazazi META. |
![]() |
Niliendelea kujisukuma taratibu na akupandisha kilima kidogo kutokea Mabatini hadi kituo cha Meta hospitali.. |
Post a Comment