Ads (728x90)








Taasisi isiyo ya Kiserikali ya ALICE FOUNDATION ya Jijini Dar es salaam kwa kushirikiana na  Wizara ya Fedha iliandaa mafunzo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini MKUKUTA kwa Maofisa watendaji na wenyeviti wa mitaa wa Kata ya Ubungo, mafunzo ambayo yalifanyika February 2012 katika ukumbi wa LEGHO Hotel Jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa taarifa kwa blog mbalimbali hapa nchini ambazo zilisambazwa kwa njia ya barua pepe na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Bi. Alice Dosi Mwamsojo ni kwamba lengo la mafunzo hayo kutoa elimu ya MKUKUTA kwa wadau wakiwemo wajasiriamali na wanasiasa na watendaji wa serikali ili kuwajengea uwezo wa kujiwezesha katika shughuli zao za kila siku.














Post a Comment