Ads (728x90)

Pichani Shule zetu - Usafi chooni inashindikana?



Choo cha shule ya msingi Lipangala, huko sehemu mojawapo ya Ludewa. Nashangaa hata kusafisha eneo linalozunguka choo ni:
  • Mbunge achangie?
  • Serikali ipangie bajeti?
  • Wazazi wachangie?
  • Walimu wahimizwe?
  • Kaka Mkuu na Dada Mkuu wa shule hawana akili timamu?
  • Elimu ya maisha na kujitegemea mashuleni imesitishwa?

Kama mambo hayo hayahitajiki kwa nini kusiwe na taratibu za wanafunzi kufanya usafi wa mazingira yao? Nahofia hapa ipo siku nyoka atakanyagwa mkia kisha kumng'ata mguu mwanafunzi.(source jamiiforums)

Post a Comment