Ads (728x90)



Mkurugenzi wa zamani wa iliyokuwa Radio Tanzania Dar es salaam,(RTD) Mzee Abul Ngarawa akizungumzia changamoto za taaluma ya habari katika zama za Utandawazi nchini.

Mzee Abdul Ngarawa akizungumza na waandishi wa habari Jijini Mbeya

Mkurugenzi Mstaafu wa RTD Mzee Abdul Ngarawa.

Mzee Abdu Ngarawa

Pamoja na uzee wake bali sauti yake mahiri na tamu ya utangazaji bado inarindima katika masikio ya wengi,

Kama ilivyo desturi ya wanataaluma ya Habari wanapokuatana bila kujali umri hakuacha kuchombeza maneno mawili matatu ya mas-hala ya kitaaluma na kuvunja mbavu kama anavyoonekana pichani akiwachekesha wanahabari.

MKURUGENZI Mstaafu wa iliyokuwa Radio Tanzania RTD Bw. Abdul Ngarawa amesema kuwa weledi wa kazi za uandishi wa habari umeporomoka kutokana na baadhi ya waandishi wa habari kutotumia vipaji vyao na badala yake kuiga sauti za watangazaji wengine kwa kukosea.
Bw. Ngarawa amesema kuwa kazi ya uandishi na utangazaji mbali ya kuwa ni taaluma bali pia inahitaji kipaji cha mtu binafsi na kwamba waandishi wanaopenda kuiga sauti za watangazaji wa zamani wanakosea.
‘’Unapaswa kutangaza wewe kama wewe ili watu wakukubali wewe kama wewe uwe na utambulisho wako mwenyewe bila kuiga lahaja na sauti za wengine,’’anasema.
Alisema kuwa watangazaji wa sasa wanapaswa kujitahidi kutangaza kulingana kutokana na mazingira ya sasa kwa kujifunza zaidi na kufuatilia vyombo vingine vya habari kwa kufuatilia sera na maadili yao kwa nia ya kuboresha taaluma na weledi katika kazi ya Uandishi wa Habari na utangazaji.
Mzee Ngarawa ameambatana na Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini TCRA ambapo pamoja na na mambo mengine watatembelea vyombo mbalimbali vya habari na Redio za FM zilizopo mkoani Mbeya ili kuibua na kupata changamoto zilizomo katika Redio hizo.

Post a Comment