Ads (728x90)


Ndugu zangu Watanzania wenzangu masikitiko makubwa saana, napenda kuchukua nafasi hii kuwatangazia habari hii nzito kwetu Kuwa Kijana Selemani aliyekuwa amevimba mguu alifariki ghafla siku ya Ijumaa saa mbili usiku nyumbani kwao Ukonga Kivule.
Utaratibu wa safari wa ndugu yetu Suleiman ulikuwa kwenye hatua za mwisho ambapo alishapata visa kwa ajili ya kwenda nchini India siku ya jumapili ya tarehe 8december kwa matibabu ila amefariki kabla ya safari yake. Aliumwa kichwa ghafla na alilalamika mbavu zinamuuma sana. Alizikwa siku ya Jumamosi. Tulimpenda mtoto Selemani,Watanzania wenzake mlionesha moyo wa upendo kwa kumchangia ili aweze pata matibabu yake ila Mungu amempenda zaidi!
Pesa zilizokusanywa kwa ajili ya matibabu yake, zitatumika kumpeleka mtoto mwingine mwenye shida kama ya Selemani anayejulikana kama Hamisi mwenye miaka 13. Tutawajuza zaidi tukiwa CCBRT kwa vipimo kabla ya safari. Asanteni na poleni sana!TAARIFA HIZI NI KWA MUJIBU WA FB YA HOYCE TEMU

Post a Comment