Ads (728x90)

Jengo la ghorofa 5 lililopo barabara ya Lupa Uhindini Jijini Mbeya linalodaiwa kujengwa kwa kutumia maji ya Wizi Mamlaka ya MAJI
Askari polisi wanaofanya doria wakioneshwa namna ambavyo wakandarasi walivyokuwa wakitumia maji bila kufungwa Mita.
Mmoja wa mafundi wanaojenga Jengo hilo akifungulia maji ambayo yameunganishwa katika mfumo wa bomba bila kufunga mita.


MAMLAKA ya maji safi na Maji Taka mkoa wa Mbeya imewanasa wakandarasi wawili wanaojenga jengo la ghorofa 5 lililopo Kitalu D barabara ya Lupa jijini Mbeya kwa kutumia maji bure bila Mita.
Hatua ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao ambao ni wakandarasi na wasimamizi wasaidizi wa jingo hilo imekuja baada ya ukaguzi unaondelea kufanywa na mamlaka hiyo juu ya matumizi halali ya Maji kwa watumiaji.
Akizungumza kukamatwa kwa Wakandarasi hao Mwanasheria wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Mbeya, Simon Bukuku alisema kuwa mnamo majira ya jioni katikati ya Jiji la Mbeya waliwanasa wakandarasi hao wakitumia maji bila kutumia mita ya Mamlaka.
Bukuku alisema kuwa hadi sasa hawajajua hasara iliyotokana na matumizi hayo ya maji kwa kuwa wamekuwa wakitumia maji hayo kwa muda mrefu tangu waanze ujenzi huo.
‘’Tutatoa taarifa za hasara iliyotokana na matumizi hayo ya maji baada ya tathmini hapo kesho,’’alisema Bukuku.
Alisema kuwa baada ya kubaini matumizi hayo ambayo ni kinyume cha sheria za matumizi ya maji waliwasiliana na vyombo vya usalama ambapo kwa msaada wa askari polisi wanaofanya doria ya Pikipiki wakawanasa watuhumiwa wawili ambao ni Bryson Mwasile na Emmanuel Mwakipesile.
Alibainisha kuwa baada ya kuwakamata wamefunguliwa kesi katika kituo cha Polisi cha Kati Jijini Mbeya kwa namba MB/IR/6563 na kwamba nyumba hiyo ambayo inaelezwa mmiliki wake kuwa ni Kanji Lalji iko katika ujenzi kwa muda mrefu.
Bukuku alisema kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa wakifanya makosa kinyume na sheria za maji na usafi wa mazingira ya mwaka 2009, kifungu cha 47 na 50.
Pia alisema kuwa makosa hayo yamao katika sheria za makosa ya Uhujumu wa Uchumi chini ya sheria za Usalama wa Taifa Cap 47, kifungu cha 3(b) na Cap 3(d) ambapo watuhumiwa ambao wanashikiliwa na polisi watafikishwa mahakamani kesho asubuhi.


Post a Comment